• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WANANCHI WAASWA KUCHANGIA UJENZI WA MAABARA MASHULENI

Posted on: April 17th, 2020

Wito umetolewa kwa wananchi kuendelea kuchangia katika miradi mbalimbali ya ujenzi inayoendelea katika maeneo yao hususani ujenzi wa maabara katika shule za sekondari kwani miradi hiyo imeonekana kusuasua ambapo kila shule ya sekondari ya kata inapaswa kuwa na maabara tatu kwa masomo ya fizikia, kemia na bailojia ambazo ujenzi wake unajengwa kwa kushirikisha nguvu ya Serikali na wananchi.

Wito huo umetolewa na Msaidizi wa Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Anza-amen Ndosa akiwa ameambatana na timu ya menejimenti ya mkoa sambamba na baadhi ya wataalam wa timu ya menejimenti ya wilaya walipokuwa katika ziara ya siku tatu ya kutembelea miradi mbalimbali ya elimu, kilimo na afya lengo ikiwa ni kuona hatua mbalimbali za miradi hiyo na changamoto zake ili kuboresha miradi hiyo iweze kufanya kazi kikamilifu.

Ndosa amesema kuwa wamebaini kuwa asilimia kubwa ya kusimama kwa miradi hiyo kumetokana na wananchi kuiachia Serikali imalizie miradi hiyo ambapo ameshauri wananchi kuendelea kuchangia miradi hiyo kwani wanafunzi wanaosoma katika shule hizo ni vizazi vyao, hivyo ni vema wakaunga mkono juhudi za Serikali kwa kuharakisha umaliziaji wa maabara hizo ili Serikali ijikite zaidi katika kuzipatia shule hizo vifaa ili wanafunzi waweze kujifunza masomo ya sayansi kwa vitendo na kwa nafasi.

MOJA YA MAABARA KATIKA SHULE YA SEKONDARI DUMILA

Akieleza athari za kutomalizika kwa maabara hizo Ndosa amesema kila shule ya sekondari inapaswa kuwa na maabara tatu kama ulivyo mwongozo kwa ajili ya masomo ya sayansi na kwamba ukosefu wa maabara hizo umechangia kwa kiasi kikubwa wanafunzi wa masomo ya mkondo wa sayansi kutofanya vizuri katika mitihani yao hivyo kupunguza uwepo wa wataalam wa sayansi ambamo ndani yake wapo madaktari, mainjinia na wataalam wengine watokanao na masomo ya sayansi.

SEHEMU YA VIFAA VYA MAABARA KATIKA MOJA YA SHULE ZA SEKONDARI

Aidha katika miradi ya kilimo hususani skimu ya umwagiliaji iliyopo katika kata ya Mvumi timu hiyo ya mkoa imeshauri Halmashauri kuendelea kutoa elimu endelevu kwa wakulima na wananchi kiujumla juu ya utunzaji wa miundombinu ya umwagiliaji ili iweze kudumu na kutumika kwa muda mrefu kwa ajili ya vizazi vijavyo.

UJENZI WA MAABARA UKIENDELEA KATIKA SHULE YA SEKONDARI MTUMBATU

Kwa upande wa miradi ya afya wameshauri Halmashauri kuanza kuandaa wataalam wa afya kwa ajili ya kituo cha afya cha Magubike ikiwemo mtaalam wa dawa za usingizi kwani katika kituo hicho ujenzi wa jengo la upasuaji unaendelea hivyo ni vema maandalizi yakafanyika mapema sambamba na maandalizi ya vifaa huku akiongeza ufanyike utaratibu wa ukarabati wa chumba cha kupumzikia mara baada ya wajawazito kufanyiwa upasuaji.

TIMU YA MKOA, TIMU YA MENEJIMENTI YA HALMASHAURI NA WATAALAM TOKA SHULE YA SEKONDARI MBUMI KATIKA PICHA YA PAMOJA.

Pamoja na hayo Ndosa na timu yake wamesema Serikali kwa sasa ina masuala mengi ya kutekeleza hususani katika kipindi hiki cha kuelekea uchumi wa kati  ambapo hakutakuwa na fedha kwa ajili ya ujenzi wa maabara hivyo waheshimiwa madiwani, watendaji wa kata na viongozi wa shule, bodi ya shule kukaana wananchi  na wadau mbalimbali ili kujadili namna ya kumalizia maabara hizo ambazo zitawajengea mazingira rafiki wanafunzi ya kujifunzia  na ufaulu wa masomo ya sayansi utaongezeka.

Licha ya kupokea ushauri, maelekezo na pongezi kwa hatua mbalimbali zilizofikiwa katika miradi iliyotembelewa katika kata za Mtumbatu, Mvumi, Dumila, Kimamba, Parakuyo, Mbumi, Mkwatani na kata nyinginezo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Mwambambale amesema kwa pamoja timu ya menejimenti ya Halmashauri ya Kilosa licha ya ukubwa wa Wilaya ya Kilosa wamepokea maelekezo na ushauri uliotolewa na timu ya mkoa na kwamba watayafanyia kazi kuhakikisha mambo yanakwenda vizuri kwani timu hiyo ipo tayari kufanya kazi kwa moyo.


Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa