• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WANANCHI WAMETAKIWA KUJITOKEZA KWA WINGI KUSHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

Posted on: September 27th, 2024

Katika kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa Wananchi Wilayani Kilosa wametakiwa kujitokeza kwa wingi kushiriki Uchaguzi huo ili kuwachagua Viongozi Bora watakaowaongoza katika Vijiji na Vitongoji vyao.

Rai hiyo imetolewa 26 Septemba 2024 na Msimamizi wa Uchaguzi Ndg. Michael .J. Gwimile wakati wa kikao cha Maelekezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ambapo amesema ni haki ya Msingi kwa kila mwananchi mwenye sifa kupiga kura na kumchagua kiongozi anayemtaka lakini pia kuchukua fomu ya kugombea nafasi za uongozi ili aweze kuchaguliwa.

Gwimile ameongeza kuwa uchaguzi huo utafanyika kwa uwazi, haki na usawa utakaozingatia sheria na taratibu zilizowekwa ambapo uchaguzi huo utalenga kuwachagua Wenyeviti wa Vijiji, Wenyeviti wa Vitongoji na Wajumbe wa Halmashauri za Vijiji katika Mamlaka ya Wilaya.

Akizungumza katika kikao hicho, Gwimile amesema zoezi la uandikishaji wa wapiga Kura utaanza kuanzia tarehe 11 hadi 20 Oktoba, 2024 ambapo uandikishaji huo utafanyika kwenye vituo vilivyopo kwenye vijiji na vitongoji husika sambasamba na  Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika taraehe 27 Novemba,2024.

Kwa upande wake Mkuu wa Polisi Wilaya  Samwel. L. Kijanga  ametoa wito kwa Viongozi wa Vyama vya Siasa na Viongozi wa Dini  kuwaelimisha wananchi  kufuata Sheria na Taratibu  zilizowekwa wakati wa zoezi la Uchaguzi ili kuepuka vitendo vya uvunjifu wa Amani katika maeneo yao, Pia amesisitiza  wananchi kutoa Taarifa endapo kutakuwa na viashiria  vya uvunjifu wa Amani ili hatua za kisheria zichukuliwe.

Naye Kamanda wa Taasisi ya kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Wilaya Gwakisa Mwaikela amewataka Viongozi wa Vyama vya Siasa, Viongozi wa Dini  pamoja na Wananchi kuzifahamu kanuni au makatazo katika kipindi hiki cha uchaguzi kama vile kupokea  au kutoa pesa, zawadi, au ahadi mbalimbali ili aweze kuchaguliwa au kujiondoa kuwa mgombea katika uchaguzi  au kushawishiwa kupiga kura zaidi ya mara moja ambavyo ni makatazo kwa mujibu wa sheria.

Kikao hicho cha Maelekezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kimeudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo Viongozi  wa  Vyama vya Siasa, Viongozi wa Dini,  Kamati ya Ulinzi na Usalama, pamoja na Wataalam wa Halmashauri.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa