• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WANANCHI WAASWA KUTOVAMIA MAENEO - DC KILOSA

Posted on: December 13th, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi ametoa rai kwa wananchi kuacha mara moja tabia ya kuvamia maeneo yaliyotaifishwa na kubatilishwa miliki mpaka hapo taratibu zote zitakapokamilika ikiwemo kufuatwa hatua stahiki kama kupitishwa kwa mapendekezo husika katika baraza la mawaziri kwa ajili ya kupitishwa kwa mujibu wa taratibu kisha maeneo hayo kugawiwa kwa mujibu wa taratibu za ugawaji ardhi zitakavyokuwa zimependekezwa.


KATIBU TAWALA WILAYA YOHANA KASITILA NA MWENYEKITI WA HALMASHAURI MH. HASSAN MKOPI NI MIONGONI MWA WAJUMBE WA KAMATI YA USHAURI

Mgoyi ametoa rai hiyo Disemba 12 wakati wa kikao cha kamati ya Ushauri Wilaya na kusema kuwa kumekuwa na baadhi ya wananchi wameamua kujimilikisha maeneo katika shamba la mwekezaji Farm Africa na kujigawia baadhi ya maeneo jambo ambalo ni kosa kisheria kwani shamba hili bado halijataifishwa kisheria, hivyo ni vema wananchi wakawa na subira hadi hapo hatua stahiki zitakapokamilika.

Pamoja na hayo ametoa onyo kwa wafugaji wanaokodisha maeneo ya ufugaji kwa wakulima jambo ambalo linaleta migogoro pindi mazao ya wakulima hao yanapostawi vizuri wafugaji hao hupitisha mifugo yao katika mashamba na kusababisha mifugo kula mazao katika mashamba na kusababisha hasara kwa wakulima na kuzua migogoro inayoleta athari ikiwemo mapigano na nyakati nyingine kusababisha vifo.

MKURUGENZI MTENDAJI WA HALAMSHAURI YA WILAYA ASAJILE MWAMBAMBALE

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Mwambambale alitumia fursa hiyo kuwakumbusha wajumbe waliohudhuria kikao hicho kuwa Halmashauri kila mwezi hutenga 10% ya mapato yake kwa ajili ya kukopesha vikundi mbalimbali vyenye sifa vya vijana 4%, wanawake 4% na wenye ulemavu 2% lengo ikiwa ni kuwasaidia kujikwamua kwa kufanya shughuli mbalimbali za maendeleo, hivyo umma utambue kuwa pesa hizo zipo na wasisite kukopa kwani zipo kwa ajili yao.

Akitoa taarifa ya usuluhishi mgogoro wa mpaka wa kijiji cha Ngaite  katika kata ya Parakuyo na kijiji cha Kwalukwambe, Malangali, Tindiga A na B kata ya Tindiga kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji, Mkuu wa idara ya Ardhi na Maliasili Cheyo Nkelege amesema kuwa kutokana na mgogoro huo uliodumi kwamda mrefu yalifanyika mazungumzo ya kutafuta suluhu ya pamoja  ambapo azimio lililofikiwa ni mpaka wa vijiji hivyo ni shamba la mifugo la NARCO uainishwe na kubaini mpaka wake ambapo kazi imeanza na kwamba bado inaendelea kwani kumebaki alama za mipaka nne ambazo hazijaonyeshwa ili kukamilisha zoezi hilo la uhakiki na ubainishaji mipaka.

Aidha kuhusu mgogoro wa mpaka kati ya kijiji cha Chaumbele A – kilichopo wilayani Kilosa na Kilama kilichopo wilayani Gairo kamati ya Ushauri Wilaya imeridhia kufanyika kwa uhakiki wa majina ya vijiji na vitongoji vyenye mgogoro, kuhakiki na kubainisha mipaka ya vijiji na mipaka ya wilaya za Gairo na Kilosa, kuepuka na kukemea ushawishi wa kisisasa unaopelekea kuwagawa wananchi kwa manufaa ya wanasiasa wachache na kuhakiki upya uanzishwaji wa vitongoji vya Mahedu kilichosajiliwa cha Kilama kilichopo Gairo na vitongoji vya Kikwajuni na Mbuyuni vilivyosajiliwa  katika kijiji cha Chaumbele kilichopo Kilosa ili kuwe na vitongoji vyenye hadhi ya kuwa vitongoji.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa