• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WANANCHI WILAYANI KILOSA WATAKIWA KUJUA NAMNA YA KUKABILIANA NA UKATILI WA KIJINSIA

Posted on: November 19th, 2024

Wananchi Wilayani Kilosa wametakiwa kutambua maana,visababishi, madhara na namna ya kukabiliana na Ukatili wa Kijinsia ili kuweza kuupunguza au kuutokomeza kabisa kuanzia ngazi ya familia, kijamii na kadhalika.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Hakiardhi Bw Cathbert Tomitho Novemba 19,2024 Wakati wa Kampeni ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia na Ukatili dhidi ya Watoto iliyofanyika katika kijiji cha Kitange ii, Kata ya Mtumbatu Wilayani humo ambapo amesema kuwa  Mila na desturi katika maeneo mengi Nchini hazimpi nafasi na uhakika mtoto wa kike kumiliki ardhi licha ya kuwa wao ndiyo walimaji na watunza familia.

Amebainisha  kuwa hali hiyo inatokana na malezi na mfumo dume ambao umekuwepo kwenye Jamii kwa miaka mingi,hivyo muda umefika wa jamii kubadilisha Mtazamo na ndiyo maana Elimu juu ya ukatili wa kijinsia inatolewa ili kila mmoja kwa nafasi yake aweze kutambua na kuelewa maana, Visababishi, na mdhara yatokanayo na ukatili huo.

Amesema kuwa lazima jamii ikemee kila aina ya Ukatili, kwa namna yeyote ile ili kujenga jamii iliyo bora hivyo anaamini kupitia mijadala mbalimbali  Wananchi wataelewa na kuweza kukabiliana na suala hilo kwani Mijadala inatoa fursa ya kila mmoja kuzungumza na kuweka maazimio ya pamoja juu ya kuondokana na Unyanyasaji katika jamii.  

Amewaasa Wananchi wasiache wala kuchoka kuripoti katika sehemu husika pindi wanapofanyiwa ukatili,au kuona mtu anafanyiwa ukatili huku akitaja baadhi ya matukio ya kikatili yaliyokithiri kwenye jamii ikiwemo ubakaji, ulawiti ,kunyimwa haki ya kusoma ,kupigwa na kadhalika.

Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya Jamii Bertila Pascal Rwehumbiza Amewasisitiza Wananchi kuripoti kwenye Madawati ya Kijinsia, kwa watu wanao waamini ikiwemo Walimu, au kupiga simu bure katika namba maalum 116 iliyotolewa na Serikali ili waweze kusikilizwa pindi wanapoona wamefanyiwa ukatili wa aina yeyote ili kuhakikisha kuwa Yule anayefanya vitendo hivyo anawajibika kwa matendo yake  na kuwa fundisho kwa wengine.

Aidha amewataka Wazazi kuacha tabia ya kuwalaza watoto chumba kimoja na jamaa au ndugu au wageni wanaokuja kuwatembelea kwani ripoti nyingi zimebainisha kuwa matukio mengi ya ubakaji yanafanywa na watu wa karibu. 

Kampeni hiyo ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia na Ukatili dhidi ya Watoto Wilayani Kilosa imefanyika kwa  ushirikiano kati ya Divisheni ya Maendeleo ya jamii na Taasisi ya Hakiardhi dhima ikiwa ni CHAGUA kutokomeza Ukatili wa Kijinsia.

 

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa