• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WANAUME WAHAMASISHA KUUPIMA VVU ILI KUTAMBUA HALI ZAO -DC KILOSA

Posted on: November 8th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa  Adam Mgoyi kupitia kampeni FURAHA YANGU - PIMA, JITAMBUE, ISHI MWANAUME JALI AFYA YAKO, PIMA VVU  amehawamasisha wanaume kupima ili kutambua hali zao za maambukizo ya VVU na kuanza ARV mapema kwa wale watakaogundulika kuwa na VVU kwani wanaume wengi wana tabia ya kumsindikiza mama apime, na akionekana yupo salama mwanaume anajiweka kwenye kundi salama jambo ambalo sio sahihi.

Mgoyi amesema kuwa kupitia Kauli mbiu ya FURAHA YANGU – PIMA, JITAMBUE, ISHI tunatupata mwongozo wa kampeni kwa kutufahamisha umuhimu wa kupima VVU, ili kujitambua na kuishi kwa furaha kwani wale wanaogundulika kuwa na maambukizi ya VVU wanapaswa kuanza dawa za kufubaza VVU (ARV) mapema na kuishi kwa furaha wakitekeleza majukumu yao binafsi, ya kifamilia na ya Kitaifa .

Aidha amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imeamua kuanzisha kampeni hii ya kuhamasisha wananchi kupima VVU, hususan wanaume, na kuanza ARV mapema mara wanapogundulika kuwa na maambukizi kama ilivyoelezwa na Waziri wa Afya, tangu Oktoba 2016, Serikali iliridhia mpango wa kupima VVU na kuanza dawa mara moja, yaani “TEST and TREAT”, bila kujali kiwango cha upungufu wa kinga ya mwili (yaani CD4). Hivyo, mpango huu una lengo la kumwanzishia dawa za ARV kila mtu aliye na maambukizo ya VVU ili aweze kuishi maisha ya FURAHA bila kuwa na hofu ya kupata magonjwa nyemelezi.

Pamoja na hayo matokeo ya awali ya Utafiti wa Nne wa viashiria vya VVU/UKIMWI (Tanzania HIV Impact Survey – THIS), uliozinduliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, katika Maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani mwaka Jana (Desemba Mosi, 2017) yanaonesha pamoja na mambo mengine kuwa hamasa miongoni mwa wananchi na hasa wanaume katika kuziendea huduma za upimaji wa VVU nchini ni ya kiwango cha chini, hivyowito kwa watu wote, husus nitoe kwenu hasa wanaume kujitokeza kwa wingi kupima VVU kwani wataalamu wapo sio tu kupima VVU bali hata magonjwa mengine sugu kama vile  uchunguzi wa awali wa Tezi Dume, Shinikizo la Damu na Uchunguzi wa Lishe

Mimi binafsi nimeamua kuwa KINARA (CHAMPION) wa kuhamasisha wanaume kupima na kuanza dawa mapema kwa wale wanaogundulika na maambukizo ya VVU. Natumia fursa hii kuujulisha umma wa jamii ya Kilosa kuwa nimeridhia kuwa KINARA WA KUHAMASISHA wanaume Wilayani Kilosa wajitokeze kwa wingi kutumia huduma hizi na ninawahamasisha viongozi wenzangu, hususan wanaume, katika   ngazi zote ikiwa ni pamoja na viongozi wa dini kutumia kauli mbiu hii kwenye majukwaa yao kuhamasisha wanaume kushiriki kikamilifu katika upimaji wa VVU na kuanza dawa mapema kwa wale wanaokutwa na maambukizi.

Aidha Mgoyi ameagiza wataalamu wa afya kupanua afua za kitabibu za uthibiti wa VVU na UKIMWI pamoja na kupanua wigo wa kuwatumia wanaogundulika na maambukizi ya VVU kuwaleta wenza wao sehemu za kupata huduma, kuimarisha fursa ya wahudumu wa afya kwa magonjwa mengine, kuwashawishi watumiaji wa huduma hizo kupimwa, kuwatumia wasanii ili kuhamasiha mabadiliko ya tabia hasa katika kupima virusi vya ukimwi mapema, kupanua huduma za upimaji na ushauri nasaha katika vituo vya kutolea huduma za afya na hata katika maeneo yenye mikusanyiko.

Pia kuainisha na kutumia maeneo ya shughuli za kiuchumi, kijamii, kidini, kimila na starehe yanayowaleta wanaume pamoja ili kuwahamasisha wanaume kuziendea huduma za upimaji wa VVU na magonjwa mengine sugu kwani utaratibu huo utaleta matokeo chanya hasa kwa kuwatumia wanaume ambao ni viongozi na wanaheshimika katika maeneo husika, kuziunganisha huduma za upimaji wa VVU katika upimaji na huduma za magonjwa mengine kama magonjwa yasiyo ya kuambukizwa ili kuimarisha upatikanaji wa huduma katika sehemu moja kwani jambo hili litawavutia wengi, hasa wanaume katika kupata huduma za upimaji wa VVU wakati wakipata huduma nyingine zenye manufaa kwa afya zao, Pia viongozi wa dini katika nyumba za ibada, wahamasishe wananchi haswa wanaume kujitokeza kwa wingi na kupima VVU na endapo wakigundulika basi waanze dawa mara moja  

      

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa