• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WANAWAKE VINARA WA LISHE WAPEWA MAFUNZO

Posted on: August 27th, 2020

Kinara wa lishe ni mtu ambaye kazi ndani ya jamii kwa lengo la kubadilisha fikra na kuleta matokeo katika lishe pamoja na kufanya ushawishi katika  mapambano dhidi ya utapiamlo kuanzia ngazi ya jamii, kitaifa, kikanda na kimataif lakini pia ana dhamira ya kubadilisha maisha ya watu, fikra na vitendo vya kuboresha hali ya lishe.

Hayo yamebainishwa na Mkufunzi wa Lishe Endelevu Harriet Mkaanga wakati wa mafunzo kwa wanawake vinara wa lishe yaliyofanyika wilayani kilosa na kusema kuwa kinara  ni shujaa katika sekta mbalimbali, kama vile siasa na michezo, lakini daima yuko tayari kutoa muda na rasilimali ili kuleta tofauti kubwa katika maisha lakini pia hutoa huduma kwa kujitolea.

 

Mkaanga amesema mwanamke kinara wa lishe anapaswa kuwa kiongozi bora ambaye yuko tayari na ana  shauku kuhusu kile kinachoweza kufanywa na anawashirikisha watu anaowaongoza, muwajibika kwa matendo yake, anaomba ushauri na kusikiliza mawazo ya wengine,Muadilifu, anajiheshimu na kuheshimu wengineo, anapatikana mda wote na anategemewa lakini pia ni mwenye maarifa na mwelewa .

Akibainisha majukumu ya mwanamke kinara amesema  anao wajibu wa kusaidia kuboresha au kupanua mipango na afua za lishe, ndani na nje ya maeneo yake, kukuza uzingatiaji ya lishe katika sekta mtambuka kama vile kilimo, mifugo, hifadhi ya jamii, kuhamasisha jamii kutekeleza majukumu  katika kukuza agenda ya lishe. kuleta watu pamoja ili wawe na lengo moja, na uwezo wa kuendesha ajenda ya lishe kwa ajili ya mabadiliko, kujihusisha katika utetezi wa jamii, harambee za kuchangisha fedha  na uhamasishaji wa rasilimali ili kuboresha lishe na kuwa na tabia chanya za lishe ili kuwa mfano wa kuigwa katika mabadiliko ya tabia ya jamii.

Akizungumzia upande wa umuhimu wa lishe bora Afisa Lishe Wilaya Zaina Kibona amesema lishe bora inasaidia kupunguza kiwango cha vifo vya watoto wachanga ambao kwa kiasi kikubwa huhusishwa na utapiamlo, Lishe bora inapunguza  viwango vya kudumaa ambayo kwa kawaida huathiri pato la Taifa, kwa wanawake ambao wako kwenye umri wa kuzaa lishe bora inasaidia kupunguza upungufu wa damu na vifo vitokanavyo na uzazi, inasaidia uzalishaji, uchumi kukua, kupunguza umaskini kwa kuboresha uwezo wa mwili kufanya kazi,  utambuzi, ufaulu shuleni, na kuimarisha afya lakini pia husaidia kupunguza  uwezekano wa kupata magonjwa sugu yasiyo ya kuambukiza  mf. kisukari, shinikizo la damu n.k.

Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 KWA SHULE ZA SEKONDARI HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOSA July 14, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI September 16, 2023
  • ZABUNI January 31, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • KILOSA KUDUMISHA USAFI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA

    September 20, 2023
  • TIMU YA UKAGUZI MKOA YATEMBELEA MIRADI YA BOOST KILOSA

    September 20, 2023
  • MAPATO YA HALMASHAURI YAONGEZEKA KUTOKA ASILIMIA 94 MPAKA ASILIMIA 98.91

    September 01, 2023
  • Walimu watakiwa kuendelea kuzifahamu huduma za kibenki

    August 29, 2023
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737-847-880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa