• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WANAWAKE WILAYANI KILOSA WATAKIWA KUTUMIA FURSA KUJIINUA KIUCHUMI

Posted on: March 5th, 2025

Katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani, Wilaya ya Kilosa imefanya maadhimisho ya kiwilaya Machi 5, 2025 katika Kijiji cha Mbwade kilichopo Kata ya Madoto ambapo Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Mhe. Shaka Hamdu Shaka, ambapo amewapongeza Wanawake kwa jitihada zao za maendeleo na kuwataka kutumia kauli mbiu ya mwaka huu inayosema "Wanawake na Wasichana 2025 Tuimarishe Haki,Usawa na Uwezeshaji" kama njia ya kujikwamua kiuchumi na kushiriki kwa haki katika uongozi wa nchi.


Akizungumza katika maadhimisho hayo, Mhe Shaka Hamdu Shaka ametoa pongezi kwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa hatua mbalimbali alizochukua katika kuhakikisha wanawake wanapata fursa nyingi za maendeleo na kwamba, fursa hizo zinapaswa kutumika kwa namna bora na kwa uzalendo, ili wanawake waweze kujenga jamii imara na kuleta maendeleo katika sekta zote za maisha

Aidha katika hotuba yake, Mhe. Shaka Mhe. Shaka amewashauri wanawake na wasichana wa Wilaya ya Kilosa kutambua nguvu waliyonayo na kuitumia vizuri kwa manufaa yao na ya jamii ambapo amesema Serikali ya Dkt Samia Suluhu Hassan itaendelea kuwaletea miradi na fursa za maendeleo, lakini pia ni jukumu lao kama Wanawake kutumia fursa hizo kwa ustawi wa familia zao na kwa maendeleo ya jamii.

 "Rais Samia amefanya kazi kubwa kwa kuwapatia wanawake fursa za kiuchumi, ikiwa ni pamoja na mikopo ya Halmashauri na miradi ya maji na hizi ni hatua kubwa ambazo zimewakomboa wanawake na kuwawezesha kujitegemea," alisema Mhe Shaka.

Aidha  Mhe. Shaka ametoa wito kwa wanawake na wasichana wa Wilaya ya Kilosa kutumia fursa zinazotolewa na serikali na ili kuwa na maisha bora na kuleta mabadiliko ya kweli huku akiwataka  kushiriki katika kugombea nafasi za mbalimbali za Uongozi, kushirikiana katika shughuli za kiuchumi, na kujitolea kwa jamii zao.

 "Wanawake wanapaswa kujitokeza kwenye nafasi za uongozi ili kuleta mabadiliko ya kweli  na wanaweza kuwa viongozi bora na wangeweza kuchukua nafasi zaidi katika serikali," alisema Mhe. Shaka. 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Haki Ardhi Kilosa, Cuthbert Tomitho, amewakumbusha wanawake kuhusu haki yao ya kumiliki ardhi huku  akisisitiza kuwa ni muhimu kwa wanawake kufahamu haki zao na kuzitumia ili kuleta maendeleo kwenye familia zao.

 "Wanawake wanapaswa kujua haki zao za kumiliki ardhi, kwani kumiliki ardhi ni haki ya msingi ya kila mmoja, na wanawake wanapaswa kutumia haki hii kujenga familia zao na kusaidia katika shughuli za kiuchumi," alisema Tomitho. 

Naye Wakili wa Taasisi ya Haki Ardhi Kilosa, Charles Ndaki, ameongeza na kusema kuwa haki  ya kumiliki ardhi ni sawa kwa wanawake na wanaume, na hakuna kizuizi cha kisheria kinachowazuia wanawake kumiliki ardhi.

"Wanawake wanastahili kuwa na haki sawa na wanaume kumiliki ardhi. Hii ni haki ya kikatiba na sheria zote za ardhi zinawawezesha kumiliki ardhi bila vikwazo yoyote," alisema Ndaki.

Kwa upande wao Wananchi wa Kijiji cha Mbwade wameishukuru Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa kwa kufanikisha sherehe hizo za Siku ya Wanawake Duniani, na kusema kuwa wamefurahi kuona kwamba wamepata Elimu ya haki zao za msingi, hususan katika kumiliki ardhi na kwamba, elimu hiyo imetoka wakati muafaka na itawasaidia kufahamu na kutafuta haki zao kwa mujibu wa sheria.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa