• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WATOTO WAKIKE WANAOFADHILIWA NA CAMFED WAASWA KUJIFUNZA STADI MBALIMBALI

Posted on: March 14th, 2020

Shirika lisilo la kiserikali linalowasaidia watoto wa kike wanaoishi katika mazingira magumu ili kuondokana na umaskini (CAMFED) limewafadhili watoto hao kupata uelewa wa kozi mbalimbali zinazotolewa katika vyuo vya ufundi ili waweze kupata hamasa ya kujifunza stadi mbalimbali zinazotolewa katika vyuo hivyo.


Hayo yamebainishwa na Katibu wa Kamati ya CAMFED Wilaya ya Kilosa Claud  Masambati wakati wa kutembelea vyuo hivyo Machi 13 mwaka huu ambapo amesema CAMFED imeamua kuwapatia watoto wa kike hamasa ya kujifunza zaidi katika vyuo vya wananchi lakini pia waweze kujua fani mbalimbali kama watoto wa kike kwani katika vyuo hivyo zipo fani ambazo wanaweza kujifunza na kuinua kipato badala ya kukaa majumbani na kushindwa kujikwamua kiuchumi ili kuepuka kuwa tegemezi.

Masambati amesema watoto hao wanaofadhiliwa na CAMFED ni wale ambao wako katika mazingira magumu ambao wanahitaji kuwezeshwa ili kuweza kujikwamua ambapo CAMFED inahusika kuwawezesha kupata elimu kutimiza ndoto zao ambapo ufadhili unaofanywa na CAMFED ni kwa watoto walioko mashuleni, waliomaliza kidato cha nne na kutaka kurudia mitihani lakini pia wanaohitaji kufanya mitihani ya QT sambamba na wale wanaotaka kujifunza masuala mbalimbali ya ujasiriamali.

Hayo yamebainishwa na Katibu wa Kamati ya CAMFED Wilaya ya Kilosa Claud  Masambati wakati wa kutembelea vyuo hivyo Machi 13 mwaka huu ambapo amesema CAMFED imeamua kuwapatia watoto wa kike hamasa ya kujifunza zaidi katika vyuo vya wananchi lakini pia waweze kujua fani mbalimbali kama watoto wa kike kwani katika vyuo hivyo zipo fani ambazo wanaweza kujifunza na kuinua kipato badala ya kukaa majumbani na kushindwa kujikwamua kiuchumi ili kuepuka kuwa tegemezi.

Masambati amesema watoto hao wanaofadhiliwa na CAMFED ni wale ambao wako katika mazingira magumu ambao wanahitaji kuwezeshwa ili kuweza kujikwamua ambapo CAMFED inahusika kuwawezesha kupata elimu kutimiza ndoto zao ambapo ufadhili unaofanywa na CAMFED ni kwa watoto walioko mashuleni, waliomaliza kidato cha nne na kutaka kurudia mitihani lakini pia wanaohitaji kufanya mitihani ya QT sambamba na wale wanaotaka kujifunza masuala mbalimbali ya ujasiriamali.


Naye mratibu wa CAMFED Wilaya ya Kilosa na Gairo Zamoyoni Salehe amesema kwa kiasi imejikita katika kumpatia mtoto wa kike elimu na kuwawezesha kufanya miradi mbalimbali kwa kupata mikopo ambayo haina riba ambayo itawasaidia kujikwamua kiuchumi na kwamba lengo la kutoa fursa ya kujikwamua ni kumfanya mtoto wa kike ajione kuwa anaweza na si kuwa tegemezi.

Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya Jamii Grace Chogogwe amewataka watoto hao wakike kuthamini ufadhili unaotolewa na CAMFED na kwamba wakati wa ujana ndio wakati wa kuumba maisha yao hivyo ujuzi wataopata wauzingatie na kuutumia vizuri katika maisha yao huku mwalimu wa chuo hicho Ginslar Ngonyani akiwataka kutumia fursa hiyo vizuri kwa kuhakikisha wapatapo mafunzo hayo kuwa na shughuli zao ili kuepuka vishawishi ambavyo hutokana na kukosa shughuli za kufanya ambapo amesema chuo cha maendeleo ya wananchi Ilonga kinatoa mafunzo mbalimbali ikiwemo ufundi uashi, ujenzi, stadi za umeme, ushonaji na nyinginezo na kwamba kinawakaribisha sana chuoni hapo ambapo mwalimu huyo pamoja na wenzake waliwatembeza watoto hao kujionea namna watoto wakike waliopo chuoni hapo wanavyojifunza na kufanya stadi mbalimbali .

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa