• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WATU WATATU WAMEFARIKI DUNIA NA WENGINE 400 WAMEBAKI BILA MAKAZI KUTOKANA NA MAFURIKO YALIYOTOKEA WILAYANI KILOSA

Posted on: December 6th, 2023

Watu watatu wamefariki dunia huku kaya zaidi ya 300 zikiarithika baada ya mvua kubwa kunyesha na kusababisha mafuriko Wilayani Kilosa ambapo kata ya Rudewa na Mvumi zimeonekana kuathirika kwa kiasi kubwa.

Hayo yamezungumzwa na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya Mhe. Shaka Hamdu Shaka Disemba 06,2023 amewataja marehemu hao kuwa ni Iddi Abdalah mwenye umri wa miaka 63 na kwamba kifo chake kimetokea baada yeye na mkewe kujaribu kuvuka mto, ndipo maji yalipomzidia na kumsomba,pia vijana wengine wawili wa kiume ambao miili yao imepatikana siku ya pili baada ya tukio hivyo kufanya idadi ya vifo hivyo kuongezeka.

Mhe Shaka amefafanua kuwa mafuriko hayo yaliyoathiri takribani  Kaya Zaidi ya 300 na kuacha mwananchi 400 bila makazi baada ya  nyumba 35 kuanguka, yamesababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha katika Mikoa ya Dodoma, Manyara na Singida hivyo kupelekea kingo za Mto Wami kubomoka na kuacha njia kisha kusababisha mafuriko hayo. 

Mhe. Shaka amesema kutokana na kadhia hiyo Serikali kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali wamefanya jitihada za awali ikiwa ni Pamoja na kutenga maeneo ya shule kwa ajili ya kuwahifadhi wahanga waliopoteza makazi yao ambapo shule ya msingi Mkondo B imetengwa kuwahudumia wahanga wa kata ya Rudewa na kwa upande wa kata ya Mvumi imetengwa shule ya Msingi Gongwe huku akiongeza kuwa Sérikali inaendelea kutoa huduma nyingine kama vile chakula, Matibabu, Umeme na maji kulingana na uhitaji.

Kwa upande mwingine Mhe Shaka ameishukuru sérikali ya Mhe. Rais  Dkt. Samia suluhu Hassan kwa kuipatia Halmashauri ya wilaya ya Kilosa kiasi cha bilioni 13 kwa ajili ya Ujenzi miundo mbinu  Kama vile mitaro na makaravati ambapo imesaidia  kutengeneza mmwagiko wa maji  kuelekea kwenye mito na kupunguza kwa kiasi kikubwa athari za mafuriko ikilinganishwa na miaka ya nyuma.

Naye Mbuge wa Jimbo la Kilosa,Profesa Palamagamba Kabudi amewataka Wahandisi wa Barabara na Maji kufanya jitihada za kurekebisha Miundombinu iliyoharibiwa na mafuriko hayo,huku akizishukuru Taasisi binafsi zilizojitolea kwa namna moja au nyingine kuwasaidia Wahanga wa mafuriko hayo.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa