• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WATUMISHI WA HAMASHAURI WATAKIWA KUFUATA SHERIA,KANUNI NA TARATIBU ZA SERIKALI

Posted on: March 27th, 2024

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Ndg Michael John Gimile amewataka Watumishi wote kufanya kazi  kwa bidii kwa kuzingatia kanuni, Sheria na taratibu zilizowekwa na Serikali lengo likiwa ni kuwaletea maendeleo Wananchi kama ilivyokusudiwa

Amesema hayo  Aprili 27, 2024 wakati wa kikao chake na Watumishi wa Divisheni na vitengo vyote kutoka Makao Makuu ya Halmashauri, kikiwa na lengo la kujitambulisha rasmi na kukumbushana masuala mbalimbali ya kiutumishi ambapo pamoja na mambo mengine amesititiza nidhamu, itifaki ya mawasiliano kazini, pamoja na haki na wajibu wa mtumishi.


Ndg Gwimile amesema kila mtumishi anapaswa kuzingatia Sheria,Taratibu na kanuni zilizowekwa na Serikali na kwamba hiyo itasaidia katika kumuongoza kufanya masuala mbalimbali pindi anapokuwa katika kutimiza majukumu yake,pia amesisitiza kuwa kila mtumishi kwa nafasi yake kusimamia taratibu zilizowekwa na kufanya kazi kwa bidii ili kuwaletea Wananchi maendeleo.

Naye Mkuu wa Divisheni ya Utawala na usimamizi wa Rasilimali watu Ndg Betuely Joseph Ruhega amesema kuwa kutokana na Wimbi la watumishi wanaostaafu Utumishi wa Umma kujikuta katika changamoto mbalimbali za kimaisha Hususan za kiuchumi mara baada ya kustaafu hali inayopelekea kupata maradhi au hata kufa amewaasa watumishi kujiandaa kustaafu mara tu wanapoanza safari yao ya ajira.

Ndg Ruhega amesema kuwa endapo Mtumishi akijiandaa mapema kiuchumi na kijamii suala la kustaafu kwa namna yeyote ile halitamsumbua hivyo amewata watumishi kujifunza kuweka akiba na kuacha tabia ya kutegemea chanzo kimoja cha mapatao kwani hiyo inapelekea watumishi wengi kuishi maisha ya kubahatisha.

 Aidha amewataka watumishi kutafuta vyanzo vingine vya mapato tofauti na mshahara ili hata wanapomaliza utumishi wao Serikalini  tayari wanakuwa wameshajikita katika jambo Fulani na hii itawaepushia kukurupuka kuingia kwenye biashara wasizokuwa na uzoefu nazo na kupelekea kuanguka kiuchumi  na wakati mwingine kuwasababishia msongo wa mawazo  au vifo vya mapema

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa