• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WAVAMIZI LANCHI YA MKATA WATAKIWA KUHAMA

Posted on: December 10th, 2018

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh. Abdallah Ulega ametoa muda wa mwezi mmoja kuanzia Desemba 10, 2018 kwa Serikali ya Wilaya ya Kilosa, Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya kwa kushirikiana na meneja wa Lanchi ya kitaifa ya Mkata iliyopo wilayani Kilosa kuhakikisha inawaondoa wavamizi wa maeneo ya lanchi, wawekezaji wasiolipa kodi pamoja na wawekezaji wanaotumia maeneo ya lanchi kinyume na taratibu.

Ulega amesema kuwa wapo wawekezaji ambao wamepewa maeneo hayo kama wawekezaji lakini wamekuwa wakiyatumia kinyume na matumizi ya maeneo hayo kwa kukodisha ili yatumike kwa kilimo ambapo kiutaratibu eneo la lanchi halipaswi kutumika kwa kilimo, hivyo ameigiza mamlaka husika kuwaondoa mara moja wawekezaji hao kwani wapo ambao wamekuwa wakilikosesha taifa pato kwa kukwepa kulipa kodi kwa ajili ya maeneo hayo na kusisitiza wakati operesheni hiyo ikifanyika ihakikishe haiwahusishi wakulima wasiohusika na kwamba wizara iko tayari kuhakikisha ajenda hiyo inafanikiwa.

Akizungumzia kuhusu mashamba pori amesema wapo watu ambao wanamiliki mashamba makubwa lakini hawayaendelezi hatua stahiki zichukuliwe dhidi ya na kwamba watu hao wataondoshwa kesho asubuhi Desemba 11, 2018 asubuhi  na kwamba katika hilo siasa iweke pembeni hatua zichukuliwe na kwamba mane ohayo ufanyike utaratibu wa kuwapatia watu watakaoyatumia kwa dhati kwa kadri inavyostahiki, sambamba na hayo amemtaka Mkuu wa Wilaya kupitia vyombo vyake vya usalama kuwaondoa watu hao kwani lanchi haitakiwi kulimwa chochote zaidi ya nyasi na kwamba maeneo hayo yanalindwa kwa mujibu wa sheria ya nyanda za malisho na chakula cha malisho na kwamba sheria hiyo ipo kuyalinda maeneo hayo.

Akisoma taarifa yake kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi, Mkuu wa Idara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Yuda Mgeni amesema  kuwa Wilaya inapendekeza hatua zifuatazo zichukuliwe ili kumaliza migogoro wilayani Kilosa ikiwemo kuiomba Wizara ya Mifugo na Uvuvi iwafute wawekezaji waliokodishiwa na kushindwa kuviendeleza vitalu vya NARCO Mkata lanchi vyenye ukubwa wa hekta 16,000, Wizara isaidie kupatikana  kwa mitambo ya kuchimba visima virefu 5 na kufukua malambo 7 jambo litakalosaidia kupunguza migogoro kwa kuwa na uhakika wa maji kwa ajili ya mifugo na kuzuia mifugo kuhama hama.

Aidha taarifa hiyo inapendekeza Wizara ya Mifugo kwa kushirikiana na Wilaya ifanye tathmini ya athari za kimazingira katika vijiji vilivyotengwa kwa malisho na kuweka mkakati wa pamoja na kurejesha uoto wa malisho, sambamba na kuiomba Wizara katika bajeti yake ya 2019/2020 itenge kiasi cha fedha kusaidia ujenzi wa lambo kubwa katika eneo la Mfilisi, Ihombwe ambalo lina hekta 34,704 ambapo kutekeleza kwa mradi huo kutapunguza migogoro na uharibifu wa vyanzo vya maji.

Akijibu mapendekezo ya taarifa hiyo Mh. Ulega amesema  mapendekezo yaliyotolewa katika  taarifa hiyo anayachukua na kuona namna ya kuyafanyia kazi kwa kujadiliana na wizara mbalimbali zinazoonekana kuguswa katika mapendekezo hayo sambamba na kuwataka wafugaji kuwa sehemu ya kuchangia katika kuleta maendeleo katika maeneo yao kwani katika miradi ya maendeleo lazima wananchi wahusike katika kuchangai kujiletea maendeleo.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa