• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Mipango
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Mifungo na Uvuvi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Wazazi wasisitizwa kuwalinda watoto kwa kuhifadhi chakula chakutosha

Posted on: June 17th, 2022

Wito umetolewa kwa wazazi na jamii kiujumla kuendelea kushirikiana na Serikali kwa kuhakikisha usalama wa watoto kwa kuimarisha ulinzi kwa kuhifadhi chakula cha kutosha ili watoto waweze kukua vizuri na kusoma vizuri kwani elimu ni bure kuanzia elimu ya msingi hadi sekondari  .

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Alhaji Majid Mwanga ambapo amemshukuru Mheshimiwa Rais Samia Suluhu kwa kuhakikisha watoto wanapata elimu bure hivyo kwa kumuunga mkono na kuendana na kaulimbiu ya Mtoto wa Afrika isemayo Tuimarishe Ulinzi wa Watoto, Tokomeza Ukatili  Dhidi Yake, Jiandae Kuhesabiwa ni lazima kila jamii ihifadhi chakula cha kutosha mwaka mzima jambo litakalosaidia kuimarisha ulinzi wa mtoto katika chakula na kumfanya mtoto kupata lishe bora ili awe na akili timamu na kuhitimu masomo yake vizuri.

Mwanga amesema kuwa mzazi kushindwa kuhifadhi chakula kwa ajili ya mtoto ni ukatili kama ulivyo ukatili wa aina nyingine hivyo kila mmoja ahahakikishe ulinzi wa mtoto unaimarishwa kwa kuhifadhi chakula cha kutosha na kwamba unapomlinda mtoto ni sawa na kulinda jamii nzima huku akiendelea kusisitiza wananchi kuendelea kujiandaa ili kushiriki zoezi la sensa ya watu na makazi inatyotarajiwa kufanyika Agosti 23 mwaka huu.

Kwa upande wake Katibu wa CCM Wilaya Comrade Shaban Mdoe amesema wazazi bado wana jukumu la kuendelea kutunza na kulinda watoto kwa kuhakikisha haki zote za mtoto zinazingatiwa ikiwemo kupata elimu, malazi, chakula, kupendwa  na kusikilizwa huku akitaka wazazi kutohusisha tofauti zao na malezi ya watoto.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii Simforosa Mollel akieleza mambo yaliyobebwa katika ujumbe wa siku ya Mtoto wa Afrika amesema kila mzazi anao wajibu wa kufahamu mwenendo wa mtoto na kuwalinda dhidi ya ukatili unaoweza kutokea dhidi ya vitendo viovu pamoja na kuhakikisha watoto wanashiriki katika zoezi la sensa kwa kuhesabiwa kwa ajili ya kuwezesha uchumi na mipango ya Taifa.

Wakisoma risala yao watoto hao wameishkuru Serikali ya aawamu ya sita kwa kuwapatia elimu bure isiyo na vikwazo kwa kujenga na kuboresha vyumba vya madarasa, nyumba za walimu, vyoo, maabara ya masomo ya sayansi, mabweni ya wanafunzi  wa kike na kiume pamoja na maktaba huku wakiiomba Serikali na mashirika binafsi kuwajengea miundombinu ya kufundishia na kujifunzia, kuboreshewa mazingira ya kujifunzia na kufundishia, ufadhili kwa watoto wanaoishi mazingira magumu na hatarishi na huduma ya chakula mashuleni, wazazi wasiotekeleza majukumu yao wachukuliwe hatua pamoja na kuwafatilia wahusika wanaowapa wanafunzi mimba.



Tangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI October 11, 2021
  • ZABUNI January 31, 2017
  • SOMA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA March 24, 2017
  • UTARATIBU WA UHAMISHO KWA WATUMISHI WA UMMA March 24, 2017
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • DC MAJID AAHIDI KUTATUA CHANGAMOTO YA UHABA WA MADAWATI

    June 22, 2022
  • Wazazi wasisitizwa kuwalinda watoto kwa kuhifadhi chakula chakutosha

    June 17, 2022
  • Vijana waaswa kuwa chachu na mfano bora wa kuigwa katika jamii

    June 15, 2022
  • Kuchangia ujenzi wa zahanati kwa kutumia kuku

    June 14, 2022
  • Angalia zote

Video

HIFADHII YA WANYAMA MIKUMI
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • MFUMO WA PLANREP

Kurasa za Mfanano

  • Tamisemi
  • Utumishi
  • NECTA
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Mkoa Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu:

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa