• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Wazazi wasisitizwa kuwalinda watoto kwa kuhifadhi chakula chakutosha

Posted on: June 17th, 2022

Wito umetolewa kwa wazazi na jamii kiujumla kuendelea kushirikiana na Serikali kwa kuhakikisha usalama wa watoto kwa kuimarisha ulinzi kwa kuhifadhi chakula cha kutosha ili watoto waweze kukua vizuri na kusoma vizuri kwani elimu ni bure kuanzia elimu ya msingi hadi sekondari  .

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Alhaji Majid Mwanga ambapo amemshukuru Mheshimiwa Rais Samia Suluhu kwa kuhakikisha watoto wanapata elimu bure hivyo kwa kumuunga mkono na kuendana na kaulimbiu ya Mtoto wa Afrika isemayo Tuimarishe Ulinzi wa Watoto, Tokomeza Ukatili  Dhidi Yake, Jiandae Kuhesabiwa ni lazima kila jamii ihifadhi chakula cha kutosha mwaka mzima jambo litakalosaidia kuimarisha ulinzi wa mtoto katika chakula na kumfanya mtoto kupata lishe bora ili awe na akili timamu na kuhitimu masomo yake vizuri.

Mwanga amesema kuwa mzazi kushindwa kuhifadhi chakula kwa ajili ya mtoto ni ukatili kama ulivyo ukatili wa aina nyingine hivyo kila mmoja ahahakikishe ulinzi wa mtoto unaimarishwa kwa kuhifadhi chakula cha kutosha na kwamba unapomlinda mtoto ni sawa na kulinda jamii nzima huku akiendelea kusisitiza wananchi kuendelea kujiandaa ili kushiriki zoezi la sensa ya watu na makazi inatyotarajiwa kufanyika Agosti 23 mwaka huu.

Kwa upande wake Katibu wa CCM Wilaya Comrade Shaban Mdoe amesema wazazi bado wana jukumu la kuendelea kutunza na kulinda watoto kwa kuhakikisha haki zote za mtoto zinazingatiwa ikiwemo kupata elimu, malazi, chakula, kupendwa  na kusikilizwa huku akitaka wazazi kutohusisha tofauti zao na malezi ya watoto.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii Simforosa Mollel akieleza mambo yaliyobebwa katika ujumbe wa siku ya Mtoto wa Afrika amesema kila mzazi anao wajibu wa kufahamu mwenendo wa mtoto na kuwalinda dhidi ya ukatili unaoweza kutokea dhidi ya vitendo viovu pamoja na kuhakikisha watoto wanashiriki katika zoezi la sensa kwa kuhesabiwa kwa ajili ya kuwezesha uchumi na mipango ya Taifa.

Wakisoma risala yao watoto hao wameishkuru Serikali ya aawamu ya sita kwa kuwapatia elimu bure isiyo na vikwazo kwa kujenga na kuboresha vyumba vya madarasa, nyumba za walimu, vyoo, maabara ya masomo ya sayansi, mabweni ya wanafunzi  wa kike na kiume pamoja na maktaba huku wakiiomba Serikali na mashirika binafsi kuwajengea miundombinu ya kufundishia na kujifunzia, kuboreshewa mazingira ya kujifunzia na kufundishia, ufadhili kwa watoto wanaoishi mazingira magumu na hatarishi na huduma ya chakula mashuleni, wazazi wasiotekeleza majukumu yao wachukuliwe hatua pamoja na kuwafatilia wahusika wanaowapa wanafunzi mimba.



Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa