• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WAZAZI WATAKIWA KUIADHIMISHA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA KWA KUBORESHA MFUMO WA MALEZI

Posted on: June 16th, 2024

Wazazi, walezi na jamii kwa ujumla wametakiwa  kuimarisha mfumo wa malezi kwa watoto wao ikiwa ni pamoja na kuwapatia mahitaji muhimu bila kubagua makundi ya watoto wenye mahitaji maalumu ili kutengeneza kizazi bora chenye tija kwa jamii na taifa kwa ujumla.

Rai hiyo imetolewa Juni 16, 2024 na Afisa Tawala kutoka Ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Kilosa Angela Mono wakati akihutubia kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya Mhe. Shaka Hamdu Shaka katika sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika ambazo Kiwilaya zimefanyika katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Zombo katika kata ya Zombo.

Bi. Mono amesema kuwa kutokana na ripoti mbalimbali kuonesha baadhi ya nchi ikiwemo Tanzania kukabiliwa na changamoto ya watoto wenye mahitaji maalum kukosa haki ya elimu au kuipata wakiwa katika mazingira yasiyo rafiki kwa hali walizonano, serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali kukabili changamoto hizo.

Miongoni mwa hatua zilizochukuliwa ni pamoja na kutunga Sera ya Elimu Jumuishi kwa watoto ambapo kutokana na sera hii hatua kadha zimechukuliwa ikiwa ni pamoja na kuwahusisha wadau na mashirika mbalimbali katika elimu, ujenzi wa miundombinu rafiki, kutoa mafunzo kwa walimu pamoja na kuandaa kampeni mbalimbali za elimu.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashari ya Wilaya ya Kilosa Mhe. Wilfred Sumari ameitaka jamii kuboresha huduma za lishe kwa watoto ili kuimarisha afya ya mwili na akili za watoto.

Aidha amewetaka wananchi kuiunga mkono serikali kwa kuwapeleka watoto shule ikiwa ni pamoja na kuwapatia mahitaji muhimu ikiwa kama vile kuwapatia huduma za afya kwani serikali ya awamu ya sita imeboresha miundombinu ya elimu na afya.

Naye mkuu wa idara ya Maendeleo ya jamii Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Alto Mbikiye akiifafanua kaulimbiu ya maadhimisho hayo, ameishauri jamii kujenga kizazi chenye maarifa pamoja na stadi mbalimbali za kazi ili ziwasaidie kujiepusha na matendo yasiyo mema kwenye jamii.

Hata hivyo, amewashauri wazazi kuwa waangalizi kwa watoto wao katika matumizi ya vifaa vya TEHAMA kama vile kompyuta na simu kwani wanaweza kukumbana na maudhui yasiyofaa kutokana na kukua kwa utandawazi.

Akitoa salamu katika maadhimisho hayo, diwani wa kata ya Zombo, Mhe. Lusinde Elias ameishukuru serikali ya wilaya kuadhimisha sherehe hizo kwenye kata yake na kuwataka wananchi wake kudumisha malezi bora kwa watoto wao.

Maadhimisho haya yanabebwa na kaulimbiu isemayo; Elimu Jumuishi Izingatie Maarifa, Maadili na Stadi za Kazi.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa