• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WAZIRI DKT. NDUMBARO AZINDUA KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA

Posted on: December 15th, 2024

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amewataka wananchi kuchangamkia fursa ya msaada wa kisheria unaotolewa bure kupitia kampeni ya Msaada wa Kisheria wa Mama Samia  ili waweze kuzijua haki zao lakini pia kuepuka migogoro mbalimbali inayokwamisha maendeleo.

Mhe. Dkt. Ndumbaro ametoa wito huo katika sherehe za uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria zilizofanyika Disemba 15, 2024 katika kata ya Magomeni.

Waziri Ndumbaro amefafanua kuwa iwapo misingi ya Usawa, Haki na Amani itadumishwa, itasaidia kuleta maendeleo kwenye jamii kwani misingi hiyo itasaidia kupunguza migogoro kwenye jamii.

Aidha amesema kuwa kampeni hii ambayo itadumu kwa siku kumi, inalenga kumaliza migogoro mbalimbali hususani migogoro ya wakulima na wafugaji na kuongeza kuwa baada ya kampeni hii, itaandaliwa ripoti ili kubainisha migogoro ambayo haijaisha ili uwekwe utaratibu maalumu wa kuimaliza migogoro hiyo.

Naye Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kilosa Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi ameishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuileta huduma hii karibu na wananchi hususani wale wasioweza kumudu gharama za kuwaajiri wanasheria pale wanapohitaji huduma za kisheria.

Aidha Mhe. Prof. Kabudi amewataka wakazi wa Kilosa kujitokeza kwa wingi kupata huduma hii ambayo itatolewa kwa siku kumi kwenye vituo tofauti tofauti.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kujifunza masuala ya kisheria katika vituo vilivyotengwa ili kuepusha wimbi la watu wanaokwenda kwenye ofisi zisizo rasmi katika kutatua migogoro hiyo.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Mhe. Shaka Hamdu Shaka ameipongeza serikali kwa kuileta huduma hii kwani itasaidia kupunguza migogoro inayoikumba jamii huku akiitaja migogoro ya ardhi pamoja na migogoro ya wakulima na wafugaji kuwa kero ndani ya wilaya ya Kilosa.

Aidha, Mhe. Shaka ameiomba serikali kuongeza muda wa kutoa huduma hii lakini pia kuongeza vituo vya kutolea huduma hii ili kukidhi mahitaji ya wilaya kutokana na ukubwa na mahitaji, siku za ziada zinahitajika.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa