• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WAZIRI MKUU APIGA MARUFUKU MATUMIZI YA KAMBA ZA PLASTIKI

Posted on: September 14th, 2021

Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa ameiagiza Wizara ya Kilimo kutoa tamko la kisera la zuio la uwepo wa matumizi  ya kamba za  plastiki nchini katika kufungashia mazao mbalimbali.

Agizo hilo limetolewa Septemba 13 mwaka huu Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro katika Mkutano wa pili wa wadau wa sekta ya Mkonge lililosomwa kupitia hotuba yake iliyosomwa na Naibu Waziri wa Kilimo Mh. Hussein Bashe ambapo amesema ili kuimarisha masoko ya ndani ni muhimu sana hivyo ni lazima kuhamasisha wawekezaji kuwekeza katika viwanda vya uongezaji mnyororo wa thamani wa zao la mkonge ili kuliendeleza zao hilo.

Aidha ameiagiza Wizara ya kilimo, bodi ya Mkonge, kituo cha utafiti Tari Mlingano na Halmashauri za Wilaya zinazolima zao hilo kuhakikisha wanafanya kazi kama timu ili kuleta mapinduzi katika zao la Mkonge nchini huku akisema lengo la Serikali katika kuongeza uzalishaji kutoka tani 37,000 zilizozalishwa kwa mwaka hadi kufikia tani 120,000 ifikapo mwaka 2025 ambapo amesema kuwa mijadala yao inapaswa kujikita katika kuboresha tija katika zao la Mkonge.

Aidha amewataka kuhakikisha wanawasaidia wakulima wadogo kutumia mbinu za kilimo bora ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wanasaidiwa kumudu utunzaji wa mashamba ili wamudu kutumia eneo dogo kwa mavuno makubwa ikiwa ni pamoja na kupatiwa mafunzo ya ugani na kuzingatia utimilivu wa idadi ya miche kwa eneo.

“hatuwezi kuongeza tija wala kufanikiwa katika kilimo cha mkonge ikiwa hakuna maeneo ya kulima zao hilo”amesema

Waziri Mkuu ameitaka bodi ya mkonge kuharakisha mchakato wa ugawaji mashamba ili wananchi wengi waweze kupata mashamba ya kulima mkonge na kwamba bodi hiyo isiishie kugawa pekee lakini pia ihakikishe wakulima wote wanalima  na kupanda kwa wakati mmoja na kuwaunganisha na wanunuzi huku akiitaka kuhakikisha inashirikiana na Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya zinazofaa kwa kilimo cha zao hilo kutenga ardhi za kilimo hicho kwa wakulima wadogo, wakubwa na wawekezaji na kwamba wanapogawa mashamba yaliyorudi kuyagawa kwa wakulima wadogo pamoja na wawekezaji wapewe mashamba kwa masharti ya kulima mkonge.

Mh.Bashe ameiagiza bodi ya mkonge ya kuwa na ofisi katika wilaya ya Kilosa lakini pia vitalu kwa ajili ya kuzalisha miche watakayowapatia wakulima pindi itakapokuwa tayari huku akiipiga marufuku NFRA kununua kamba za plastiki kwa ajili ya kufungia magunia badala yake wanunue kamba za katani na kwamba gunia za katani ndizo zitatumika hivyo tenda yoyote itakayohitaji vifungashio kipaumbele kitakuwa katika magunia ya katani na Wilaya ya Kilosa itapata sapoti ya kutosha ili kukuza zao la mkonge.

Wakieleza changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo katika zao la mkonge Mwenyekiti wa wadau wa zao la mkonge Damian Luhinda na Mwenyekiti wa bodi ya mkonge Bi Mariam Mkumbi wamesema miongoni mwa changamoto wanazokutana nazo ni ukosefu wa mitaji, ushindani  wa bidhaa za plastiki, kuongezeka kwa gharama za mashamba(kodi), uvamizi wa tembo mashambani na matumizi makubwa ya kamba bandia ambazo ni tofauti na kamba za mkonge pamoja na  tembo  ambao wamekuwa wakiharibu zao la mkonge likiwa lingali shambani na kusababisha hasara kwa wakulima hivyo wameiomba Serikali kudhibiti uzalishwaji na matumizi ya kamba bandia kwani uwepo  wa matumizi ya kamba bandia unaua soko la kamba stahiki lakini pia wameiomba Serikali kudhibiti vurugu zinazofanywa na tembo.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa