• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WILAYA YA KILOSA YAADHIMISHA SIKU YA MISITU DUNIANI NA UPANDAJI MITI KITAIFA KWA KUPANDA MITI 2000

Posted on: March 22nd, 2025

Katika kuadhimisha Siku ya Misitu Duniani na Siku Ya upandaji Miti Kitaifa, Wilaya ya Kilosa leo Machi 22,2025 imefanikisha tukio la kihistoria kwa kupanda Miti elfu mbili katika Shule ya Sekondari Mazinyungu, ikiwa ni sehemu ya Juhudi za Serikali kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa misitu na utunzaji wa mazingira.

Afisa Maliasili na Hifadhi ya Mazingira wilaya ya Kilosa, Hamis Nzunda, amewahimiza wananchi kuendelea kushiriki katika juhudi za kupanda miti ili kufikia lengo la serikali la kupanda miti milioni 1.5 kwa kila halmashauri ifikapo mwaka 2025.

“Leo tumepanda miti elfu mbili, lakini kazi bado ni kubwa,tutashirikiana na wadau wengine kuhakikisha tunafikia malengo yetu na kufanya Kilosa kuwa mfano wa utunzaji wa mazingira,” alisema Nzunda.


Naye Afisa kutoka Mamlaka ya Misitu Tanzania (TFS), Hilda Mwalongo amesema sherehe hizo huadhimishwa kila Mwaka Tarehe 21,Machi  ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali kuhamasisha wananchi kuhusu faida ya misitu na umuhimu wa kuhifadhi mazingira na kwamba ushirikiano baina ya TFS na Serikali na mzuri katika utunzaji wa mazingira na kusema kuwa  wametoa miche elfu mbili kwa jamii ya kwaajili ya kufanikisha Zoezi hilo katika Wilaya ya Kilosa.


Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Kilosa, Prof. Palamagamba Kabudi, ameitaka jamii kuhakikisha wanajitolea kutunza miti ili kuweza kupata manufaa ya mazingira, huku akiwasisitiza Wananchi  kuiunga mkono kwa vitendo Kaulimbiu ya mwaka huu 2025 isemayo” Ongeza Thamani ya Mazao ya Misitu kwa Kizazi cha Sasa na Kijacho”

“Misitu ni Rasilimali muhimu kwa ustawi wa jamii na ikiwa hatutahakikisha tunalinda misitu yetu, tutakuwa na athari kubwa za mazingira kama ukame na mabadiliko ya hali ya hewa,” alisema Kabudi, akiongeza kuwa jamii lazima itambue faida zinazopatikana kwa kuendelea kutunza mazingira.


Mgeni Rasmi katika maadhimisho hayo Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Mhe. Shaka Hamdu Shaka, amewapongeza Wananchi kwa kushirikiana na Serikali katika juhudi za kupanda miti, akisema kuwa Misitu ni biashara inayoweza kuleta maendeleo kwa jamii.

“Mabadiliko ya hali ya hewa na uhaba wa rasilimali ni changamoto kubwa. Misitu ni biashara, na uvunaji wa hewa mkaa na mazao mengine ya misitu inaweza kuwa chanzo cha mapato kwa wananchi wa Kilosa na wananchi wanapaswa kutambua kuwa utunzaji wa misitu ni uwekezaji wa baadaye kwa vizazi vijavyo,” alisisitiza Shaka.

Kwa upande mwingine, Wananchi wameishukuru Serikali kwa kuanzisha shughuli hiyo ya kupanda Miti na kuhamasisha umma kuhusu  kutunza mazingira na kwamba elimu waliyopata itawawezesha kuwa na uelewa mkubwa wa faida za misitu na jinsi ya kuitunza ili iweze kutoa huduma endelevu kwa jamii.

Tangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA WAHE. MADIWANI May 22, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • WAUGUZI WATAKIWA KUWA WAADILIFU MAHALI PA KAZI

    May 30, 2025
  • WAHE. MADIWANI WAISHUKURU SERIKALI YA AWAMU YA SITA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    May 30, 2025
  • KILOSA YAJIPANGA KUTATUA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI

    May 28, 2025
  • VITENGO VYA HABARI SERIKALINI VIIMARISHWE KWA KUFANYA MAWASILIANO YA KIMKAKATI

    May 24, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa