• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WODI MPYA YA WAZAZI HOSPITALI YA WILAYA YAANZA KUTUMIKA

Posted on: January 22nd, 2020

Katika kuinua sekta ya afya Wilaya ya Kilosa imeimarisha huduma za afya kwa kuimarisha huduma za uzazi kwa wanawake na kinamama wajawazito kwa kufungua wodi mpya ya wazazi ambayo imeanza kufanya kazi na kutoa huduma kwa kinamama wajawazito na waliojifungua ambayo imeboreshwa na kutegemewa kutoa huduma zote katika jengo moja tofauti na jengo la awali.

MKUU WA KITENGO CHA WODI YA WAZAZI BI SARA ELIAH AKIWA OFISINI KWAKE

Hayo yamebainishwa Januari 22 mwaka huu na  Mkuu wa kitengo cha Wodi ya Wazazi  katika hospitali ya Wilaya Sarah Eliah ambapo amesema kuwa wodi hiyo imeanza kazi Januari 21 mwaka huu ambapo amesema kuanza kutumika kwa wodi  hiyo kumekuwa mkombozi kwa kiasi kikubwa kutokana na changamoto mbalimbali zilizokuwa zinawakabili kiutendaji kazi, kinamama wajawazito na kinamama waliojifungua kwani jengo la awali lilikuwa dogo, chakavu na lisilotosheleza kihuduma pia baadhi ya miundombinu yake haikuwa bora na kuvuja baadhi ya maeneo  tofauti na jengo la sasa ambalo ni kubwa na linatarajiwa kutoa huduma muhimu za kinamama kwa urahisi katika jengo moja.


MMOJA WA WAUGUZI AKIWA KATIKA MAJUKUMU YAKE KATIKA WODI YA WAZAZI


Bi Elia amesema pamoja na jengo kujitosheleza zipo baadhi ya changamoto ikiwemo ufinyu wa vyumba  kwa ajili ya kinamama wanaojisubiria kujifungua kuwa vichache na vidogo, miundombinu ya umeme bado haijakaa sawa kuwa na umeme wa kutosheleza kwa jengo zima, miundombinu  kwajili ya kubebea wakinamama kabla ya kuwapeleka chumba cha upasuaji kwa ajili ya kujifungua ambapo kwa sasa kinamama wajawazito wanaopaswa kujifungua kwa njia ya upasuaji wanalazimika kutembea kwenda jengo la upasuaji pamoja na nguvu ya maji kuwa ndogo kipindi ambacho hakuna umeme.

Licha ya changamoto hizo ameushukuru uongozi wa Wilaya kwa hatua zilizofikiwa na juhudi zilizoonyeshwa katika kuboresha huduma za afya ambapo pia ameshauri kuongezwa kwa vyumba vingine viwili ili kuweza kukidhi mahitaji ya wateja kwani zipo nyakati ambazo hupokea wakina mama wajawazito wengi takribani 10 hadi 15 kwa siku hivyo kwa hali hiyo itapelekea kuwa na uhaba wa vyumba, aidha amesema upande wa vyoo katika jengo hilo jipya ni vya kutosha hivyo kupelekea kinamama kuwa salama kiafya dhidi ya magonjwa mbalimbali ya maambukizi tofauti na jengo la awali ambalo shimo la choo lilikuwa ni moja.


BAADHI YA KINA MAMA WAJAWAZITO WANAOJISUBIRIA KUJIFUNGUA WAKIWA WODINI

Kwa upande wa kinamama wajawazito na wazazi waliolazwa katika wodi hiyo kwa nyakati tofauti wameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa na Wizara ya Afya kwa ajili ya wodi hiyo kwani mazingira ni mazuri na huduma ni nzuri ambazo wameanza kuzipata lakini pia lina nafasi ya kutosha lakini pia kwasasa usumbufu haupo uliokuwa ukitokana na ndugu waliokuwa wakiingia wodini na kusababisha kelele na usumbufu kwa wauguzi kwani kwa sasa ndugu wote huishia nje ya wodi lakini pia wamesema awali wajawazito na waliojifungua kwa njia ya kawaida walikuwa wanakaa eneo moja lakini kwa sasa hali tofauti ambapo wanaojisubiria wana eneo lao halikadhalika waliojifungua pia wana eneo lao.

BAADHI YA KINAMAMA WALIOJIFUNGUA WAKIWA NA WATOTO WAO KATIKA WODI YA WAZAZI

Kwa upande wa kinamama wajawazito na wazazi waliolazwa katika wodi hiyo kwa nyakati tofauti wameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa na Wizara ya Afya kwa ajili ya wodi hiyo kwani mazingira ni mazuri na huduma ni nzuri ambazo wameanza kuzipata lakini pia lina nafasi ya kutosha lakini pia kwasasa usumbufu haupo uliokuwa ukitokana na ndugu waliokuwa wakiingia wodini na kusababisha kelele na usumbufu kwa wauguzi kwani kwa sasa ndugu wote huishia nje ya wodi lakini pia wamesema awali wajawazito na waliojifungua kwa njia ya kawaida walikuwa wanakaa eneo moja lakini kwa sasa hali tofauti ambapo wanaojisubiria wana eneo lao halikadhalika waliojifungua pia wana eneo lao.

JENGO JIPYA LA WODI YA WAZAZI KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA KILOSA


Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa