• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

WORLDVISION YAKABIDHI MADAWATI, CHEREHANI NA KADI ZA BIMA KWA WILAYA YA KILOSA

Posted on: October 7th, 2020

Uongozi wa Wilaya ya Kilosa umeushukuru uongozi wa taasisi ya World vision kwa mchango wao ambao wamekuwa wakiutoa kupitia miradi mbalimbali ambayo wamekuwa wakiifanya katika sekta ya elimu, afya, maji,kilimo, uchumi, uongozi,  maendeleo pamoja  na  ufadhili wa watoto.

Shukrani hizo zimetolewa Oktoba 6 mwaka huu na Katibu Tawala Wilaya Yohana Kasitila wakati akipokea madawati 100 kwa ajili ya shule ya msingi Mtumbatu pamoja na kadi za bima kwa watoto 2,910 pamoja na cherehani 35 kwa ajili ya vijana waliojifunza ujasiriamali vyote vikiwa na thamani ya shilingi 31,475,000.

Kasitila amesema kazi iliyofanywa na World Vision ni kubwa kwa ajili ya maendeleo ya wanakilosa na inastahili kupongezwa kwani vifaa hivyo vitakuwa msaada mkubwa hususani kwa kizazi cha sasa na baadaye na kwamba vifaa hivyo vimepunguza changamoto ya wanafunzi kukaa chini lakini pia upande wa vyerehani vitakwenda kuwasaidia vijana kujitegemea na kujikwamua kiuchumi huku kadi za bima zitasaidia watoto kupata huduma za afya bila usumbufu.

Aidha ametoa rai kwa Serikali ya kijiji na wananchi kiujumla kuwatazama wazee na wasiojiweza ili waweze kupata bima ya afya na kwamba ili uchumi kuimarika unahitaji watu wenye afya bora na elimu hivyo ipo haja ya wananchi kujipanga namna ya kuendeleza mema yote yaliyofanywa na World Vision ambao wanatarajia kumaliza muda wao ifikapo tarehe 30/09/2021.

Naye mwakilishi kutoka World Vision Bw. Kulanga amesema kutokana na kutambua juhudi zinazofanya na Serikali World Vision imejikita katika kuunga mkono juhudi hizo hususani kwa kuboresha miundombinu ya shule ikiwemo ujenzi wa madarasa, nyumba za walimu na ofisi pamoja na ujenzi wa vyoo, kuijengea jamii uwezo juu ya afya ya mama na mtoto, lishe, usafi binafsi na wa mazingira, uchimbaji na ukarabati wa visima vifupi vya maji, kuwajengea uwezo jamii juu ya mbinu bora za kilimo na ufugaji ili kuongeza uzalishaji na kipato pamoja na kuwezesha upatikanaji wa mbegu bora , pembejeo lakini pia mafunzo ya ujasiriamali, uanzishwaji na uendeshwaji wa vikundi vya kuweka na kukopa na mambo mengine mengi.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa