• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

ZAIDI YA WATOTO 108,000 WAPEWA TIBA KINGA

Posted on: February 28th, 2020

Zaidi ya watoto 108,000 walio na umri wa kwenda shule wilayani Kilosa Mkoani Mororogo wamepewa dawa kama tibakinga kwa magonjwa ya kichocho na minyoo  ambayo yalikuwa hayapewi kipaumbele ili kuwakinga wasiathiriwe na magonjwa hayo.

Hayo yameelezwa  Februari 25 mwaka huu na Mratibu wa mpango wa kudhibiti magonjwa ambayo yalikuwa hayapewi kipaumbele Halmashauri ya Wilaya Kilosa  Rosemary Nguruwe katika ziara yake ya kutembelea shule mbalimbali za msingi ambazo zilitumika kama kituo cha kumezea dawa na kuona zoezi la umezaji dawa linavyofanyika  .

Nguruwe amesema kuwa zoezi hilo limefanyika kwa muda wa siku tatu kuanzia Februari 24 hadi 26 mwaka huu na limekwenda vizuri  kwani  walimu na wazazi wameonyesha ushirikiano wa kutosha kwa kufanya maandalizi ya kutosha na  kuwapa  chakula   watoto kabla ya kumeza dawa  jambo ambalo limepelekea zoezi hilo  kuwa na mvuto wa kipekee na kufanya zoezi la  umezaji dawa kukamilika  katika kila kituo.

Hata hivyo amewapongeza na kuwashukuru walimu kwa ushirikiano wao ambapo amesema kuwa  Idara ya Afya na Elimu zinafanya kazi pamoja katika kuihudumia jamii na kwamba kazi kubwa waliyoifanya kuhakikisha watoto wote walioko mashuleni wanameza dawa sahihi kulingana na kipimo, na kuongeza kuwa  kwa kazi kubwa waliyoifanya wameisaidia  Serikali kupitia Wizara ya Afya  kufanikisha zoezi hilo  kwani   Serikali  ina mpango wa kutokomeza magonjwa yote ambayo yalikuwa hayapewi kipaumbele kama vile minyoo na kichocho.

Aidha walimu katika shule mbalimbali  akiwemo Mkuu wa shule ya msingi Mkondoa Annastasia Hemed  amesema zoezi hilo ni zuri na ni muhimu kufanyika mara kwa mara ili kuepuka madhara yanayoweza kutokea kupitia magonjwa hayo kwa kuwa linasaidia kuwaondolea changamoto watoto na ndio waathirika wakubwa kutokana   na mazingira  na vyakula wanavyokula hasa wawapo shuleni hivyo ni  rahisi kupata vimelea vya magonjwa hayo, hivyo  wameishauri Serikali kutoa dawa hizo mara kwa mara ambapo itasaidia watoto wote kumeza kwa muda muafaka.

Nao wanafunzi kwa nyakati tofauti wameeleza kuwa wanaishukuru Idara ya Afya kupitia Halmashauri ya Wilaya Kilosa kwa kuwathamini na kuwapelekea dawa hizo mashuleni na kwamba hawana uwezo wa kuzipata dawa hizo kwa wakati ukizingatia kwao ni  rahisi kupata vimelea vya magonjwa hayo kulingana na changamoto ya mazingira.

Kwa upande wa Madaktari katika vituo vya Afya na Zahanati wamesema dawa hizo hazina madhara yeyote kwa mtoto na kwamba wazazi hawana budi kumpeleka mtoto mwenye sifa katika kituo cha kumezea dawa ili aweze kupata tiba kinga ili kujihakikishia usalama wa afya ya mtoto dhidi ya magojwa hayo.

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa