• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

ZIARA YA KAMATI YA SIASA MKOA KATIKA TARAFA YA MAGOLE

Posted on: November 20th, 2023

Mbunge wa jimbo la Kilosa kwa kushirikiana na waheshimiwa madiwani wa tarafa ya Magole wametoa shukrani za dhati kwa Serikali ya awamu ya sita kwa namna ambavyo imekuwa ikiitazama Wilaya ya Kilosa kwa jicho la tatu kwa kuhakikisha inawaletea wananchi maendeleo sambamba na kuhakikisha inatekeleza yale iliyo yaahidi wakati wa kampeni za uchaguzi ikiwemo utatuzi wa kero mbalimbali.

Shukrani hizo zimetolewa mwishoni mwa wiki hii wakati wa ziara ya kamati ya CCM Mkoa ilipotembelea tarafa hiyo ili kuzungumza na wananchi ambapo Mbunge wa jimbo la Kilosa Mh Prof. Palamagamba Kabudi amesema Serikali imekuwa ikitoa fedha nyingi kwa ajili ya utatuzi wa changamoto mbalimbali ikiwemo changamoto ya maji ambapo takribani shilingi milioni 97 zimetolewa na Serikali ili kuunganisha kisima cha Matongolo kwenda kwenye tanki la maji.

Aidha Prof Kabudi amewataka wananchi wote kwa aujumla kuendelea kutunza vyanzo vya maji kwa kuhakikisha miti haikatwi hovyo na kuchoma mkaa, kutokakata magugu na mikuyu, jambo linalosababisha kuwa na uhaba wa maji na kwamba kila mmoja ahakikishe miti inapandwa ya kutosha ili kuwepo na upatikanaji wa maji kwani Serikali inafanya juhudi za kuleta maji kwa wananchi ili kuondoa adha ya uhaba wa maji.

Pamoja na hayo ametoa rai kwa wananchi kuzichukua changamoto na kuzigeuza kuwa fursa ya kujiletea maendeleo kwa kuunga mkono juhudi za Serikali katika utatuzi wa changamoto na kwamba changamoto la umeme Serikali imeshatoa fedha kwa vijiji vyote kupewa umeme na kwamba inatarajiwa ifikapo mwezi Disemba 30, 2023 vijiji vyote nchini viwe na umeme na kwamba Serikali imejipanga baada ya kumaliza suala la umeme vijijini itaanza mchakato wa upatikanaji wa nishati safi ya kupikia.

Kwa upande wa madiwani wa kata za tarafa ya Magole ikiwemo Mvumi, Msowero, Kitete, Dumila, Magole, Mbigiri, Mamboya, Maguha, Mabula, Mtumbatu, Magubike na Berega wamemshuru Mheshiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa fedha mbalimbali zilizopelekwa na zinazoendelea kupelekwa kwenye kata zao ili kuwasaidia wananchi ambapo kumekuwa na miradi mbalimbali inayoendelea ikiwemo ujenzi wa vituo vya afya na zahananti, ujenzi wa shule na miundombinu mbalimbali sambamba na miradi mingine mingi.



Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MRADI WA SHULE YA SEKONDARI MASANZE

    May 20, 2025
  • WATENDAJI NGAZI YA HALMASHAURI WATAKIWA KUWA WAADILIFU

    May 14, 2025
  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa