• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

ZINGATIENI MATUMIZI BORA YA ARDHI

Posted on: February 26th, 2018

                 

Imebainika kuwa shirika la kuhifadhi misitu ya asili Tanzania (TFSG) kwa kushirikiana na Mtandao wa Jamii wa Usimamizi wa Misitu Tanzania (MJUMITA) kupitia mradi wa mkaa endelevu umeonekana kuwa na tija hasa katika kukuza ushirikiano na mahusiano yanayolenga kuboresha uwezo wa wanachama wake wa kujihusisha kwa ukamilifu na usimamizi na uhifadhi wa misitu, kutetea kuongezeka kwa umiliki na matumizi bora ya ardhi na misitu kwa ajili ya kuboresha maisha ya jamii.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi wakati wa uzinduzi wa Maonyesho ya Wazi ya Shughuli za Mradi wa Mkaa Endelevu na miradi ya maendeleo katika kijiji cha Ulaya Mbuyuni wilayani Kilosa ambapo amesema kuwa Mungu ametutunukia bahati ambayo tunapaswa kuitunza na kuitumia vizuri huku tukizingatia kanuni na sheria za matumizi bora ya ardhi kwani hakuna jambo zuri linaloweza kufanyika bila mpangilio.

Mgoyi amesema ni vema sheria na matumizi bora ya ardhi yakazingatiwa  na kutumika inavyopaswa, hivyo kila kiongozi afanye majukumu yake kwa kusimamia misitu isikatwe hovyo bali kwa kuzingatia ushauri unaotolewa na wataalamu kutoka TFSG na MJUMITA kwani kwa kufanya hivyo migogoro haitakuwepo, ambapo katika maonyesho hayo Mkuu wa Wilaya ametembelea msitu wa hifadhi ya kijiji cha Ulaya Mbuyuni na eneo lililotengwa kwa ajili ya uzalishaji mkaa endelevu na kuzindua  kisima cha maji.

Sambamba na hayo Meneja Mradi wa Mkaa Endelevu Bw.Charles Leonard amesema mradi wa mkaa endelevu kwa sasa wilayani  Kilosa unafanya kazi katika vijiji ishirini vya Kisanga, Msimba, Ihombwe, Kitunduweta, Mhenda, Kigunga, Ulaya Mbuyuni, Ulaya Kibaoni, Dodoma Isanga, Nyali,Unone, Rudewa Gongoni, Mvumi, Makwambe, Gongwe, Kisongwe, Chabima, Mbamba, Mfuluni na  Zombo.........

Tangazo

  • TANGAZO LA KONGAMANO LA VIJANA WILAYANI KILOSA April 04, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAMETAKIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUBORESHA TAARIFA ZAO

    May 07, 2025
  • RC MALIMA AWATAKA WAAJIRI MOROGORO KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI WAO

    May 01, 2025
  • WALIMU WAPYA 74 WILAYANI KILOSA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KUHUSU MAADILI NA HAKI ZA UTUMISHI WA UMMA

    April 29, 2025
  • KILOSA YABORESHA USIMAMIZI NA UFATILIAJI WA MIKOPO YA 10% KWA UNUNUZI WA GARI JIPYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa