• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

Zingatieni uadilifu na uwazi kuwabaini walengwa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini - DC Kilosa

Posted on: July 7th, 2021

Wawezeshaji wa mpango wa kunusuru kaya maskini(TASAF) ngazi ya Wilaya kwa kushirikiana na madiwani pamoja na viongozi katika ngazi ya vijiji  wametakiwa kuhakikisha wanawatambua walengwa sahihi wa mpango wa kunusuru kaya maskini(TASAF) waliokusudiwa na kuhakikisha kazi hiyo inafanyika kwa uadilifu na uwazi badala ya kuweka wanufaika hewa kwa kuweka majina ama kaya zisizostahili kwani lengo la mpango huo ni kumsaidia mwananchi maskini.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa alhaji Majid Mwanga ambapo amewataka kuhakikisha wanatimiza mwongozo unavyoelekeza na kwamba kila mmoja atambue kuwa anakwenda kuwakilisha Serikali hivyo miradi itakayoibuliwa iwe na mwendelezo ambayo itawanufaisha walengwa na jamii kiujumla ambapo pia ametaka katika shughuli mbalimbali kushirikishwa kwa maafisa tarafa kwani kwa kufanya hivyo itasaidia shughuli hizo kusonga mbele.

Janeth Maduhu ambaye ni mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji TASAF amesema tathmini ya utekelezaji wa mpango wa kunusuru kaya maskini katika kipindi cha kwanza cha awamu ya tatu  umepungua kutokana na walengwa kujiimarisha katika kufanya shughuli mbalimbali za kijiongezea kipato na kujiimarisha kiuchumi  kwa kufanya shughuli za kilimo, ufugaji, uvuvi na ujasiriamali ambapo awali baadhi ya vijiji vilifikiwa na kwamba katika awamu hii ya pili vijiji vyote vitafikiwa.

Kwa upande wake Waziri wa Katiba na Sheria ambaye pia ni mbunge wa Kilosa Kati Mh. Prof.Palamagamba Kabudi amesema fedha zinazotolewa na mpango huo sio za bure bali kwa ajili ya kuwasaidia walengwa ili kuziondoa kaya lengwa katika umaskini hatimaye waweze kujikwamua na kuchangia pato la Serikali kwani mpango huo umekusudia kuifanya jamii kujikwamua hivyo ni vema washiriki wote watakaoshiriki kuwabaini walengwa kujikita katika uadilifu na uwazi ambapo pia ametaka wananchi washirikishwe katika mchakato huo huku akisisitiza walengwa wote watakaobainika na kuingia katika mpango huo wanapaswa kuzifanyia kazi fedha watakazopatiwa kwa kuhakikisha wanajikwamua na kutoka katika lindi la umaskini kwani mpango huo sio wa kudumu.  

Naye mbunge wa jimbo la Mikumi Mh. Dennis Londo amesema ipo haja ya kuongeza umakini na kuzingatia vigezo katika kuwabaini walengwa ili kuboresha utekelezaji wa mpango huo kwa kuwazingatia wanufaika wa masharti ambao watakuwa wamekidhi vigezo ambapo pia amewataka viongozi hao kuhamasisha jamii ili kunufaika na mpango huo kwa kuhakikisha wanatimiza vigezo vyote ikiwemo kupeleka watoto kliniki na watoto wote wanaostahili kwenda shuleni  huku akiitaka jamii kutambua kuwa mradi huo sio wa kudumu hivyo ni vema jamii ikapata ushauri mzuri na kuuzingatia ili kuleta mabadiliko kwa walengwanna kuondokana na umaskini.




Tangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA WAHE. MADIWANI May 22, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • WAUGUZI WATAKIWA KUWA WAADILIFU MAHALI PA KAZI

    May 30, 2025
  • WAHE. MADIWANI WAISHUKURU SERIKALI YA AWAMU YA SITA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    May 30, 2025
  • KILOSA YAJIPANGA KUTATUA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI

    May 28, 2025
  • VITENGO VYA HABARI SERIKALINI VIIMARISHWE KWA KUFANYA MAWASILIANO YA KIMKAKATI

    May 24, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa