• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Dawati la Malalamiko |
KILOSA DISTRICT COUNCIL
KILOSA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Divisheni
      • Utawala,Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu ya Awali na Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Miundombinu ya Mijini na Vijijini
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu
      • Fedha na Uhasibu
      • Maliasili na Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
        • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba Mbalimbali
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Jarida la Mtandaoni
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Tangazo
    • Maktaba
    • Hotuba
    • Vyombo vya Habari
    • Video

ZOEZI LA UGAWAJI VITAMBULISHO WAJASIRIAMALI WADOGO LINAHITAJI UADILIFU- DC KILOSA

Posted on: December 31st, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi ametoa rai kwa watendaji wote wa kata wilayani Kilosa kuweka maslahi ya Taifa mbele badala ya matakwa yao binafsi katika zoezi zima la utambuzi wa wafanyabiashara walio katika sekta isiyo rasmi kwa ajili ya ugawaji wa vitambulisho vilivyotolewa kwa wafanyabiashara wadogo wadogo ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Mheshimia Rais ambapo uzinduzi wa ugawaji wa vitambulisho hivyo utafanyika tarehe 4 Januari 2019.

Mgoyi amesema kuwa watendaji wote wanawajibika kufanya zoezi la utambuzi wa wafanyabiashara wadogo wadogo kwa kuzingatia uadilifu wa hali ya juu ili kutoingia katika dosari ya aina yoyote na kwamba mtendaji yoyote asithubutu kutumia udanganyifu katika zoezi hilo kwani kwani zoezi linalohitaji uangalifu wa hali ya juu ili kuepuka ukwepaji kodi kwa kuwasilisha majina yasiyostahili huku akiwataka kuepuka rushwa kwani zoezi hili si la kisiasa bali kiutendaji na ni agizo kutoka kwa Rais hivyo libebwe kwa uzito wake na heshima ya Rais na kwamba mtendaji yoyote atakayebainika kufanya udanganyifu sheria itachukua mkondo wake.

Aidha Mgoyi amesema kuwa Wilaya inaendeshwa kwa kilimo hivyo  amewataka watendaji hao kuhakikisha maafisa kilimo waliopo katika kata zao wanawajibika ipasavyo ili kwenda sambamba na agizo la Waziri Mkuu la kuwataka Wakurugenzi wote nchini wahakikishe maafisa ugani wawe katika maeneo ya wakulima ili kuwasaidia, hivyo watendaji wanaowajibu kusimamia vizuri maafisa hao na kwamba kila mtendaji anapaswa kuwa na daftari la wakulima ili kuwa na takwimu sahihi za wakulima, mazao yanayolimwa pamoja na hekari zinazolimwa katika maeneo yao.

Akisoma mwongozo wa kugawa vitambulisho kwa sekta isiyo rasmi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri ya Wilaya ya Kilosa Asajile Lucas Mambambale amesema mfanyabiashara anayestahili kupewa kitambulisho sharti awe na mauzo ghafi yasiyozidi shilingi milioni nne (4,000,000/=) kwa mwaka, awe hajawahi kusajiliwa na TRA na kupewa Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN) isipokuwa wale waliosajiliwa awali na kupata kitambulisho au kama Mlipakodi, anatakiwa ajaze fomu maalum kama mfanyabiashara wa sekta isiyo rasmi mathalan mama lishe, mmachinga na pia mjasiriamali atalipa shilingi elfu ishirini(20,000/=) kwa ajili ya kitambulisho

Sambamba na hayo Asajile amewataka watendaji wa kata kutofumbia macho sekta ya kilimo kani wao ndio wasimamizi wakuu katika maeneo yao katika sekta ya elimu ambapo kwa miaka kadhaa kilosa imekuwa ikishika nafasi ya mwisho kimkoa na kwamba 2019 hatarajii sekta ya elimu katika mitihani ya Taifa  kushika nafasi ya mwisho kimkoa na amewataka watendaji hao kukaa na serikali za maeneo yao kupanga mikakati ya kuitoa Kilosa katika nafasi ya mwisho kwa kupandisha kiwango cha ufaulu ili kushika nafasi nzuri kimkoa kwani ni jambo linalowezekana.

Naye Kaimu Meneja TRA Kilosa Musa Haruni ni vema watendaji wa kata na jamii kiujumla ikaelewa kwa kina kuwa walengwa wa vitambulisho hivyo ni wale ambao wanapata mauzo kwa mwaka bila kujali faida wala mtaji wastani wa mauzo ni 11,111.01/= ambapo mauzo kiwango cha chini ni 5000/= huku kikubwa kikiwa 18000/= kwa siku aidha amesema kwa upande wa wafanyabiashara ambao hawajasaliwa na TRA wala hawana TIN lakini ni wafanyabiashara wanaozidi milioni nne kwa mwaka hawapaswi kupewa vitambulisho.

Tangazo

  • TANGAZO LA MKUTANO WA BARAZA LA WAHE. MADIWANI May 22, 2025
  • Tangazo la kuanzishwa Dawati Maalum la kushughulikia Migogoro ya Wakulima na Wafugaji November 13, 2024
  • Tangazo la Dawati la Msaada wa Kisheria November 13, 2024
  • TANGAZO LA BARAZA LA MADIWANI LA RISIMU NA MAPENDEKEZO YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 February 25, 2025
  • Angalia zote

Habari za sasa

  • WAUGUZI WATAKIWA KUWA WAADILIFU MAHALI PA KAZI

    May 30, 2025
  • WAHE. MADIWANI WAISHUKURU SERIKALI YA AWAMU YA SITA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    May 30, 2025
  • KILOSA YAJIPANGA KUTATUA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI

    May 28, 2025
  • VITENGO VYA HABARI SERIKALINI VIIMARISHWE KWA KUFANYA MAWASILIANO YA KIMKAKATI

    May 24, 2025
  • Angalia zote

Video

RAIS SAMIA ATENGA BILIONI 7.2 KUENDELEZA BONDE LA RUHEMBE
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • e-Mrejesho
  • CHF ILIYOBORESHWA
  • MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA
  • MFUMO WA FFARS
  • MFUMO WA PLANREP
  • MFUMO WA KIBALI KUSAFIRI NJE YA NCHI

Kurasa za Mfanano

  • e-Mrejesho
  • Mkoa Morogoro
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Jamhuri ya Muungano Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo la Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Kilosa

    Sanduku la posta: S.L.P 65 Kilosa

    Simu: 023 2623093

    Simu: 0737847880

    Barua Pepe: ded@kilosadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hatimiliki imehifadhiwa ©2017 Halmashauri ya Wilaya Kilosa